• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Babati District Council
Babati District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango Ufuatiliaji na Takwimu
      • Ardhi mali Asili na Wanyamapori
      • Maendeleo ya jamii na ustawi wa jamii
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mazingira na Usafi wa Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji nyuki
      • Teknologia ya Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Uchaguzi
    • Link ya Machapisho ya Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kiofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Zoezi la Utambuzi na Utoaji Chanjo Laanza Rasmi Mkoani Manyara

Posted on: July 3rd, 2025

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza Rasmi kutekeleza Mpango kabambe wa Kampeni ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo Kitaifa, ambapo leo imetoa chanjo kwa mifugo takribani 400 ili kuboresha na kuleta mabadiliko makubwa katika Sekta ya Mifugo na kuondoa vikwazo ambavyo vimekuwa vikizuia Mifugo na mazao yake kuuzwa katika nchi zenye Masoko mazuri.Akizungumza katika zoezi la Uhamasishaji na Utoaji Chanjo za Mifugo leo Julai 3, 2025 Wilayani Babati Mkoani Manyara, Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Babati ambaye ndiye alikuwa Mgeni Rasmi wa zoezi la Uhamasishaji na Utoaji wa Chanjo za Mifugo Wilayani hapo, na Katibu Tawala Wilaya ya Babati, Ndg. Thobias Abwaro amesema zoezi la Utoaji Chanjo na Utambuzi wa Mifugo ni zoezi endelevu ambalo ni la muda mrefu na litaleta tija kwa wafugaji na Taifa zima kwa ujumla.“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kugharamia Mpango wa Utoaji chanjo na Utambuzi wa Mifugo kwa miaka 5 kutoka 2025 hadi 2029, ambao utagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 216 za Kitanzania, na ametoa ruzuku ya asilimia mia Moja kwa chanjo za kuku ambayo ni sawa na bure, na asilimia 50% kwa chanjo za ng'ombe na mbuzi/kondoo, ambapo ng'ombe ni  tshs. 500/= na mbuzi/kondoo ni tshs. 300/=, hii yote ni kuonesha ni jinsi gani anajali Mifugo  na Wafugaji.” ameseama Ndg. Abwaro Aidha, Ndg. Abwaro amesema kwa muda mrefu uchanjaji wa Mifugo umekuwa ukifanyika kidogo kidogo katika ngazi za Mamlaka ya Serikali za Mitaa, mashamba makubwa na wafugaji mmoja mmoja bila kuwa na uratibu wa pamoja ambao hauwezi kutokomeza Magonjwa hayo ya Mifugo, kwani ili kutokomeza Magonjwa hayo inabidi kuchanja Mifugo angalau kwa asilimia 70%.Vilevile, Ndg. Abwaro kwa niaba ya wafugaji wa Mkoa wa Manyara amemshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia na kutoa Ruzuku ya Kampeni ya Chanjo za Mifugo ambayo inaenda kuwanufaisha wafugaji na kuwaletea tija Kibiashara.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Prof. Erick Komba, amesema kuwa Mifugo inaathiriwa sana na magonjwa mbalimbali ambayo yanapelekea vifo vya Mifugo na mazao yake kutokuwa bora na hata kupelekea kutokidhi viwango vya Masoko ya nje."Ndio maana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia na kuiwezesha Sekta hii ili kuboresha maisha ya Mifugo na wafugaji, na kutanua wigo wa Masoko ya nje" amesema Prof. KombaPia, Prof. Komba amesema kuwa ni Imani yake kuwa zoezi hili litafanikiwa kwa asilimia mia Moja na chanjo hizi zitasaidia kuimarisha Mifugo na hatimae kuwa na mazao Bora zaidi.Halikadhalika, Prof. Komba amewataka wafugaji kujitokeza kwa wingi katika kuchanja Mifugo yao ili kutokomeza  Magonjwa hayo ya Mifugo kwani Kampeni hii ni fursa adhimu kwa wafugaji.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA UANDIKISHAJI WAPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 25, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 03, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI WASIMAMIZI VITUO VYA WAPIGA KURA June 30, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI 2020 June 17, 2020
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC Manyara Akagua Miradi ya Zaidi ya Bilioni Sita Babati DC

    July 03, 2025
  • Zoezi la Utambuzi na Utoaji Chanjo Laanza Rasmi Mkoani Manyara

    July 03, 2025
  • Ujenzi wa Nyumba za Walimu Manyara Boys, Matunda ya Rais Samia

    July 01, 2025
  • Jamii Imetakiwa Kutumia Vyakula Vyenye Virutubisho

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MAKALA YA ELIMU IKIANGAZIA SWALA LA TAALUMA NA HALI YA UFAULU KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BABATI
video zaidi

Viunga vya haraka

  • Watumishi portal
  • Lgrcis dashborad
  • Salary silpportal
  • Ramani ya Halmashauri

Tovuti Mbalimbali

  • Tovuti ya Ofisi ya Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Ofisi ya Raisi,Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa-TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Wilaya Ya Kiteto
  • Secretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya wilaya ya Babati

    Anwani: P.O BOX 400, Babati.

    Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011

    Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577

    Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani Ya Tovuti

Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.