Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Anna Mbogo ameiomba jamii kuwapeleka watoto wote wenye mahitaji maalumu shule ili wapate elimu. Mkurugenzi ameyasema hayo leo alipowatembelea watoto wenye Mahitaji maalum katika shule ya Msingi Dareda kati iliyoko kata ya Ayalagaya " Nimekuja kuwasalimia watoto wangu walioko bweni nasisitiza jamii ipeleke watoto wenye mahitaji maalum shuleni wakapata elimu" amesisitiza kiongozi huyo.Wakati huohuo Bi. Mbogo ametumia fursa hiyo kugawa viatu vilivyotolewa na Rais Mhe Samia Suluhu Hassan kupitia Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao inayoendesha Kampeini ya Samia Nivishe Viatu kwa ajili ya watoto wenye Mahitaji maalum wa shule ya Msingi Dareda kati . Watoto wenye mahitaji Maalum wakionesha furaha yao wamemkumbatia Mkurugenzi wakisema kwa sauti wanamshukuru Rais Samia. Serikali kwa kushirikiana na Wananchi, na Wadau mbalimbali wamejenga bweni la watoto wenye mahitaji maalum katika shule hiyo na linatumika.
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.