• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Babati District Council
Babati District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango Ufuatiliaji na Takwimu
      • Ardhi mali Asili na Wanyamapori
      • Maendeleo ya jamii na ustawi wa jamii
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mazingira na Usafi wa Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji nyuki
      • Teknologia ya Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Uchaguzi
    • Link ya Machapisho ya Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kiofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

BILIONI 9.88 KUJENGA LAMI BARABARA YA DAREDA MJINI - DAREDA MISSION BABATI

Posted on: April 13th, 2024

BILIONI 9.88 KUJENGA LAMI BARABARA YA DAREDA MJINI -  DAREDA MISSION BABATI


Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemuagiza Mtendaji Mkuu Wakala wa Barabara (TANROADS) kumsimamia Mkandarasi kampuni ya Jiangxi Geo Engineering kukamilisha kwa wakati ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Dareda hadi Dongobesh (km 60) sehemu ya kwanza ya Dareda Mjini hadi Dareda Missioni (km 7) ili kuufungua kiuchumi Mkoa wa Manyara.


Bashungwa amezungumza hayo Wilayani Babati Mkoani Manyara Aprili 06, 2024 wakati akishuhudia utiaji saini mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo kati ya Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS) na kampuni ya M/s Jiangxi Geo Engineering (Group) Corporation ya China kwa gharama ya Shilingi Billioni 9.88.


“Tumempa Mkandarasi huyu kwa kuwa tayari anatekeleza miradi mingine ya barabara maeneo haya na jirani na tumemuongezea hii nyingine kwa kuwa si kilometa nyingi hivyo Mtendaji Mkuu sitaki kusikia visingizio nataka barabara hiyo ikamilike haraka maana hata Wakandarasi wa ndani kilometa saba wangeweza kuzijenga”, amesisitiza Bashungwa.


Bashungwa amemtaka Mkandarasi huyo kuhakikisha anakamilisha ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Labay-Haydom (km25) na barabara ya Mbulu-Garbabi (km 25) ambapo Serikali inakwenda kulipa madeni ambayo alikuwa anayadai ili miradi yote iweze kukamilishwa kwa haraka.


Aidha, Bashungwa amempongeza Mtendaji Mkuu wa TANROADS kwa kutekeleza maagizo ya Wizara ya kutolimbikiza kazi nyingi kwa Mkandarasi mmoja na hivyo miradi mingi kuchelewa na kusababishia hasara Serikali.


“Nikupongeze Mtendaji Mkuu kwa kutumia hatua za kimkataba kumuondoa Mkandarasi wa barabara ya Lukuyufusi - Mkenda Mkoani Ruvuma mara baada ya kuona hafanyi vizuri kwenye maeneo mengine”, amesema Bashungwa.


Bashungwa amempongeza Mtendaji Mkuu wa TANROADS kwa kusimamia ushiriki wa Wahandisi Washauri wa ndani katika usimamizi wa miradi ambapo katika mradi huu usimamizi utatekelezwa kupitia Kitengo cha Usimamizi wa Miradi cha TANROADS (TECU).


Naye, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendinga amesema mradi huu unapita katika Wilaya ya Mbulu na Babati na ujenzi wa barabara hii inakwenda kuongeza thamani ya mazao ya shamba ikiwemo kilimo na ufugaji pia itarahisisha wananchi kufanya biashara pembezoni mwa barabara na kukuza uchumi wa mkulima mmoja mmoja na Mkoa kwa ujumla.


Vilevile, Sendinga ameomba Bajeti ya kimkakati kwa ajili ya matengenezo ya barabara kwa ajili ya Mkoa wa Manyara kutokana na Mkoa huo kuwa na mvua kubwa za mara kwa mara na kuleta athari kubwa ya miundombinu ya barabara.


Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo ameeleza kuwa wananchi wa Babati wamekuwa wakisubiria barabara hiyo kwa hamu sana ambapo ikikamilika itasaidia kukuza uchumi wa wana Babati na Mkoa wa Manyara kutokana na uzalishaji mkubwa wa kilimo unaofanyika.


Mtendaji Mkuu wa Wakala wa TANROADS, Mhandisi Mohamed Besta amesema Mkandarasi aliyeshinda zabuni ni kampuni ya M/s Jiangxi Geo Engineering (Group) Corporation ya China, kwa gharama ya Shilingi Billioni 9.88 ambapo utasimamiwa na Wataalamu wa ndani katika kitengo cha Usimamizi (TECU).


Besta ameongeza kuwa zabuni kwa ajili ya ujenzi wa sehemu ya pili ya Dareda Mission – Dongobesh (Km 53) inatarajiwa kutangazwa katika Mwaka huu wa fedha 2023/24.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA UANDIKISHAJI WAPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 25, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 03, 2024
  • TANGAZO LA UKODISHAJI VIBANDA KITUO CHA AFYA MAGUGU January 09, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI 2020 June 17, 2020
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Viongozi wa Kisiasa Wakubali Kutoa Elimu Awamu ya Pili Daftari la Wapiga Kura

    May 08, 2025
  • Wajumbe wa Baraza la Madiwani Waishukuru Serikali

    May 07, 2025
  • Wananchi Jitokeze Kuboresha Taarifa Kwenye Zoezi la Uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

    May 07, 2025
  • Kituo Cha Afya Gallapo Kimepata Gari la Wagonjwa

    May 07, 2025
  • Angalia zote

Video

MAKALA YA ELIMU IKIANGAZIA SWALA LA TAALUMA NA HALI YA UFAULU KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BABATI
video zaidi

Viunga vya haraka

  • Watumishi portal
  • Lgrcis dashborad
  • Salary silpportal
  • Ramani ya Halmashauri

Tovuti Mbalimbali

  • Tovuti ya Ofisi ya Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Ofisi ya Raisi,Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa-TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Wilaya Ya Kiteto
  • Secretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya wilaya ya Babati

    Anwani: P.O BOX 400, Babati.

    Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011

    Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577

    Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani Ya Tovuti

Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.