Viongozi wa kuchaguliwa wametakiwa kuwatumikia wananchi wote bila kubagua tofauti zao ili kuwaletea maendeleo katika maeneo yao. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange kwenye Mkutano wa kusikiliza na kutatua kero uliofanyika leo ofisi za Kijiji cha Hyasem kata ya Ayalagaya H/ Wilaya ya Babati. " viongozi wasikilizeni wananchi wote bila kuwabagua" amesisitiza kiongozi huyo. Katika Mkutano huo wananchi wamelalamika kuwa Mwenyekiti wa Kijiji hicho Ndg Martin Safari haitishi vikao vya kisheria, anatumia, madaraka yake vibaya na anakwamisha shughuli za maendeleo katika kijiji hicho. Naye Mkuu wa Wilaya amewaeleza wananchi kuwa kwa siku zilizobaki mwenyekiti huyo ajitathimini kama kweli anaongoza kijiji hicho kwa kufuata sheria kanuni na taratibu. Mhe. Twange kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa H/ Wilaya Babati, Meneja TANESCO , Meneja TARURA na Meneja RUWASA wametatua kero mbalimbali za wananchi na ziara ya Mkuu wa Wilaya ya kutatua kero kijiji cha kijiji inaendelea
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.