Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoani Manyara itaendelea kushirikiana na Mashirika yasio ya Kiserikali (NGOs) katika kupambana na umasikini na kuwaletea maendeleo Wananchi . Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ndg . Benedict Ntabagi leo kwenye kikao cha wadau wa maendeleo kilichofanyika ofisi za Makao ya Halmashauri ya Wilaya ya Babati" Halmashauri ya Wilaya ya Babati itaendelea kushirikiana na NGOs katika kupambana na umasikini wote tuungane pamoja" amesisitiza kiongozi huyo. Katika taarifa yake iliyosomwa na Afisa Maendeleo ya Jamii Ndg January Bikuba amesisitiza NGOs kujikita kuwezesha Wananchi katika utunzaji wa mazingira ikiwa ni pamoja na kutoa Elimu na upandaji miti kwa vitendo na kuwaeleza kila wanapokutana na changamoto katika kutekeleza kazi zao wasisite kuwasiliana na ofsi ya Mkurugenzi ili itatuliwe. Halmashauri ya Wilaya ya Babati imejiwekea utaratibu Kila robo mwaka inakutana na Wadau wa maendeleo kwa lengo la kujadili taarifa ya utekelezaji na kuweka Mpango mkakati kwa kazi zitakazofanyika kwa robo mwaka unaofuata.
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.