Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoani Manyara inatarajia kukusanya na kutumia kiasi chaTsh 59,091,932,000 kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Wakijadili na kupitisha mapendekezo ya makadirio ya mpango na bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2024/2025 leo kwenye mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika Makao Makuu ya H/Wilaya ya Babati, Mwenyekiti wa Baraza la hilo Mhe, John Noya amesema bajeti hiyo imeongezeka kwa asilimia 14 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka jana ya makisio ya Tsh 51,927,333,000ya mwaka 2023/2024. Mhe.Noya ameongeza kuwa ongezeko hilo limetokana na kuongezeka kwa bajeti ya makusanyo ya mapato ya ndani, mishahara ya watumishi,wadau wa maendeleo, na michango ya wananchi.Mhe Noya ametumia fursa hiyo kuwashukuru Madiwani, Watumishi wadau wa maendeleo na wananchi kwa kazi na ushirikiano katika kuchangia miradi na shughuli za maendeo.Wakati huohuo Mkurugenzi Mtendaji wa H/ Wilaya ya Babati Anna Mbogo amepongeza Serikali kuu kuendelea kuleta fedha ili kukamilisha miradi ya maendeleo
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.