Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange ameagiza H/ Wilaya ya Babati kusimamia miradi ya Afya iliyopewa fedha na serikali kuu ikamilike kwa wakati na ianze kutoa huduma kwa wananchi. Mhe. Twange ameyasema hayo leo wakati akitoa taarifa ya Serikali kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani H/ Wilaya ya Babati uliofanyika ofisi za Makao Makuu Dareda. "Nafahamu serikali kuu imeleta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vitatu ( 3) vya Afya vya Ayasanda, Bashnet, na Madunga ongezeni kasi ktk ujenzi wa vituo hivyo vikamilike kwa wakati wananchi wapate huduma.Aidha amesisitiza madiwani wa kata hiyo kusimamia miradi hiyo ijengwe kwa viwango vinavyotakiwa.Katika Mkutano huo Mhe. Twange amesisitiza wananchi kuishi kwa amani bila kubaguana na kufanya kazi kwa bidii hasa kilimo ktk kipindi hiki cha mvua.
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.