Mkuu wa Wilaya ya Babati Mh Elizabeth Kitundu amewataka Wananchi wa Wilaya ya Babati kukamilisha miundombinu ya Ujenzi wa madarasa kabla ya Mwezi desemba 2018 ili watoto wote waliofahulu Mtihani wa darasa la saba Mwaka 2018 waweze kuingia kidato cha kwanza Januari mwaka 2019. Mkuu wa Wilaya ameyasema hayo leo kwenye Mkutano wa Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Babati kujadili taarifa za kata uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati "Waheshimiwa Madiwani ni jukumu lenu lá kuhamasisha Jamii ili itoe michango kukamilisha ujenzi wa madarasa ya kidato cha kwanza katika maeneo yenu" amesisitiza Mkuu wa Wilaya. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mhe. Nicodemus Tarmo naye amewaomba Wahe. Madiwani kwenda kuhamasisha jamii kukamilisha ujenzi wa madarasa hayo kwani jukumu la kujenga miundombinu ya Shule ni lá Jamii yenyewe. Aidha Mkuu wa Wilaya ya Babati amewaomba wahe. Madiwani kwenda kuwajulisha Wazazi wa watoto wote walifahulu kuhakikisha wanawasimamia ili waweze kwenda shule kidato cha kwanza mwaka 2019. Matokeo ya Mtihani wa Darasa la saba mwaka 2018 yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani, Halmashauri ya Wilaya ya Babati imefahulisha Kwa asilimia 78.37 na imekuwa Halmashauri ya 2 Kimkoa kati ya Halmashauri 7 za Mkoa wa Manyara na imeshika nafasi ya 93 Kitaifa kati ya Halmashauri 186 zilizofanya Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi mwaka 2018.
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.