Shule za sekondari Ayalagaya, Dareda pamoja na Madunga ambazo ni shule za kata katika Halmashauri ya wilaya ya babati zimeingia katika kumi bora kimkoa kwa shule zilizofanya vizuri katika matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2022 yaliyotangazwa tarehe 29.1.2023.
Shule ya sekondari Ayalagaya ikishika nafasi ya tatu kimkoa, shule ya sekondari Dareda nafasi ya tano huku shule ya sekondari Madunga ikishika nafasi ya sita.Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Babati amewapongeza walimu, wanafunzi pamoja na Maafisa Elimu kwa ushirikiano na kazi kubwa wanayoifanya katika kuboresha Hali ya Taaluma katika Halmashauri ya wilaya ya Babati.
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.