Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati Anna Mbogo ameishukuru Taasisi ya Mama ongea na Mwanao inayoendesha Kampeini ya Samia Nivishe Viatu kwa kutoa viatu kwa wanafunzi wa shule za Msingi za Gallapo na Endanoga . Akipokea viatu hivyo leo kutoka kwa taasisi hiyo kwa nyakati tofauti katika shule za Msingi za Gallapo na Endanoga na kuvikabidhi, Mkurugenzi Mbogo kwa niaba ya Wazazi ameishukuru Taasisi hiyo kwa kutoa viatu katika shule hizo zilizopo kata ya Gallapo Halmashauri ya Wilaya Babati.Mkurugenzi Mbogo ametumia fursa hiyo kumshukuru Mhe .Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa fedha anazotoa katika ujenzi wa miradi katika Halmashauri ya wilaya ya Babati akitoa mfano fedha Tsh 180 Milion zilizotolewa kukarabati shule ya Msingi Kongwe ya Gallapo.Naye Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Ndg Steven Nyerere amesisitiza wanafunzi hao kusoma kwa bidii na kufanya katika masomo yao.Hafla ya kampeini ya Samia Nivishe viatu imehudhuriwa na Viongozi ,wananchi ,walimu na wanafunzi wa shule hizo kwa ujumla wote wamepongeza
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.