Kituo Cha Afya Madunga kilichojengwa na Serikali katika Kijiji Cha Gidngwar kata ya Madunga H/Wilaya ya Babati kimeanza kutoa huduma.
Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Madunga leo Daktari Kiongozi wa H/ Wilaya ya Babati Dkt Hosea Madama amesema Huduma zitakazotolewa kwanza ni huduma ya Wagonjwa wa Nje, Maabara, huduma ya Mama na Mtoto na kujifungua. Aidha amesema Huduma za upasuaji na Wodi za wazazi zitaanza mara baada ya majengo yanaendelea kujengwa kukamilika. Akitoa neno la shukurani Kwa niaba ya Wananchi wa Kata ya Madunga, Diwani wa Kata hiyo ambaye ni Mwenyekiti wa H/Wilaya ya Babati ameshukuru serikali Kwa kutoa fedha kiasi Cha Tsh 250 Millioni ( tozo ya miamala ) Kwa ujenzi wa kituo hicho na kuwashukuru Wananchi wa Kata yake Kwa michango na nguvu kazi mpaka kukamilika na kutoa huduma katika Kata hiyo " Sisi tunafuraha kuona kituo kilichojengwa na Serikali Kwa kushirikiana na Wananchi kinaanza kutoa huduma kwa ukaribu na Wananchi amesisitiza kiongozi huyo.
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.