Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati umewataka Wawekezaji wenye Mashamba Makubwa kulima kilimo cha kisasa, chenye tija na kulipa kodi zote za serikali zinazostahi kwa wakati. Hayo ameyasema Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mhe. John Noya kwenye Kikao cha pamoja kati ya Wawekezaji hao na Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya kilichofanyika leo katika ukumbi wa Halmashauri ya Babati kwa lengo kujadili mapato ya Halmashauri yatokanayo na Mashamba makubwa pamoja na matumizi ya Ardhi katika mashamba hayo. "Tumewaita wawekezaji ili kujua kwanini hawalipi kodi zinazostahili kwa serikali pia kujua kwa nini baadhi ya Mashamba hayalimwi na kusikiliza changamoto zenu ili kuongeza mapato ya Halmashauri " amesisitiza Makamu Mwenyekiti. Aidha Makamu Mwenyekiti amesisitiza kila Mwekezaji awe amelipa Kodi mbalimbali na madeni yake kabla ya tarehe 10/12/2018. Mwekezaji wa Shamba lá Odedra Plantation Ndg. Odedra D kwa niaba ya Wawekezaji wengine ameshukuru kwa wito huo na kuhaidi kulipa kodi za serikali zote kwa wakati na kisha akaomba Halmashauri isaidie kuhamasisha kilimo cha Miwa ili wananchi walime miwa kwa wingi kwa ajili ya kiwanda chá Manyara sugar kilichoko Matufa Halmashauri ya Wilaya ya Babati kipate malighafi. Afisa Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji Ndg Jetrida Kyekaka amewaomba wawekezaji hao kulima mazao ya Biashara yenye soko Mfano Pamba lenye Kiwanda cha Hanang Cotton Mill kilichoko Kijiji cha Mawemairo kata ya Magugu Halmashauri ya Wilaya ya Babati na akasema zao hilo lina soko lá uhakika na bei iko juu.
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.