Baraza la Madiwani la H/ Wilaya ya Babati limejadili na kupitisha mapendekezo ya Makadirio ya Mpango na Bajeti ya Mapato na Matumizi ya kiasi Tsh 62,092,419,436 Kwa mwaka fedha 2023/2024. Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Mhe. John Noya leo kwenye Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani wa kujadili wa kujadili Mpango na Bajeti ya Mwaka 2023/2024 uliofanyika leo katika Ukumbi wa H/ Wilaya ya Babati. Mwenyekiti huyo amesema Kiasi Cha Tsh 3,445,000,000 ni fedha kutoka mapato ya ndani na kiasi kinachobaki nifedha kutoka Serikali kuu, wadau wa maendeleo na Wananchi. Mwenyekiti huyo amewataka Madiwani kwenda kwenye Kata na Vijiji kufanya vikao na Wananchi kuwaeleza kazi nzuri zinazofanywa na Serikali hasa Kwa kutoa fedha za miradi Kwa Kila Kata, kwenda kusimamia miradi ijengwe kwa ubora unaotakiwa na kudhibiti Matumizi mabaya ya fedha. Mkurugenzi Mtendaji wa H/ Wilaya Anna Mbogo ameshukuru Serikali Kwa kuendelea kutoa fedha za ujenzi wa Miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati .
Halmashauri ya wilaya ya Babati
Anwani: P.O BOX 400, Babati.
Simu ya mezani: Simu Na. 027-2531011
Simu ya Kiganjani: 0620444641,075486577
Barua pepe: info@babatidc.go.tz,ded@babatidc.go.tz
Copyright ©2020 Babati District Council . All rights reserved.